Jumamosi, 13 Septemba 2014

SILAHA ZA VITA KATIKA MAISHA YA KIROHO.



             SILAHA ZA VITA KATIKA MAISHA YA KIROHO.

Silaha ni vifaa vinavyotumika wakati wa vita na kuleta ushindi.

Mpendwa unapompokea Yesu kuwa bwana mwokozi wa maisha yako na kuanza kuishi maisha ya kiroho unakuwa umetangaza vita katika ulimwengu wa roho.maana yake umeokolewa kutoka katika mikono ya shetani kuanzia hapo shetani anaanza kukutafuta ili akurudishe kwenye ulimwengu wa kipepo ili uukose uzima wa milele.na kama ndiyo umeokoka tu vita huanza kupitia watu wako wajirani na wa muhim ili kukuyumbisha mfano vita huanza kupitia wazazi kutokubaliana na maamuzi yako na kukufukuza au kutokukusomesha na vitisho vya aina nyingi ili ukate tamaa.usikate tamaa kwa sababu ya majaribu kwa sababu Mungu hukutana na watoto wake wakati wa matatizo.hata Yesu mwenyewe alikatariwa tangu yupo tumboni hata mariam akakosa mahali pa kujihifadhi ni vita za shetani kuharibu kusudi la Mungu lakini kwa sababu Mungu ni mwenye kutunza ahadi na ni wa ushindi Yesu alizaliwa na na aliitangaza kweli na alinyeyekea mpaka mwisho na sasa kainuliwa yupo upande wa kuume wa MUNGU BABA na amepewa mamlaka.USIKATE TAMAA  YASHINDE MAJARIBU ILI UINULIWE.

Leo nataka tujifunze baadhi ya silaha za vita tulizopewa na Mungu ili tushinde.


Efeso 6:14,basi simameni,hali mmejifunga kweli viunoni na kuvaa dirii ya ya haki kifuani,na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa injiri ya amani,zaidi ya yote mkiitwa ngao ya imani ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya Yule mwovu. Sehem zilizopigiwa mstari ni silaha ambazo zinakuwezesha kutangaza ushuhuda wa kweli na ushindi.

·         Kweli humfanya mtu kuwa huru na ukisha kuwa huru  vita lazima utavishinda maana yake hauna jambo lolota linalokufanya usijiamini,haki ni uhusiano mzui yrtu na mungu,nyoofu wa kweli mbele za Mungu

·         Neno la Mungu,efeso6:17 neno la Mungu ni upanga wa roho linakata kila aina ya uharibifu unaotaka kumpoteza mtu katika maisha ya kiroho.yeremia23:29 je! neno langu si kama moto?aseme bwana na kama nyundo ivunjayo mawe vipande vipande. Mathayo4:3 Pia shetani alimjaribu Yesu lakini kwa sababu Yesu alijawa na neno la Mungu alimshinda shetani kwamba mtu haishi kwa mkate tu ila ni kwa neno litokalokatika kinywa cha Mungu.kumbe neno   la Mungu ni uzima na ni njia ya kumshinda mwovu.usipokuwa na neno la Mungu, utamjibu mwenzio vibaya,utatukana,utakata tamaa kwa sababu ya vitisho vya mwovu.soma neno la Mungu umshinde shetani.

·        
Jina la Yesu,tunatakiwa kulitumia jina la yesu katika vita ili kuharibu majeshi maelfu ya shetani,pia kufungua Baraka,kupatanishwa na Mungu,katika kila jambo tunalolifanya yafaa liwe katika jina la yeu ndipo tutamwona Mungu akitushindia.(tunalitumia jina la Yesu ili Baba yaani (MUNGU) atukuzwe kupitia mwana ambaye ndiye Yesu).(filipi2:9 Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno,akamkirimia jina lile lipitalo kila jina ,ili kwa jina la yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni na vya duniani,na vya chini ya nchi.na kila ulimi ukiri ya kuwa ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA,kwa utukufu wa MUNGU BABA)Mungu alimpa jina ambalo litafanyika ushindi kwa wote watakao mwamini.

·         Damu ya Yesu,ufunuo wa yohana12:11 Nao wakamshinda kwa damu ya mwana kondoo na kwa neno la ushuhuda wao…kumbe tunashinda vita kwa damu ya mwana kondoo nae Yesu kristo,

·         Sifa kuu ni silaha,kumsifu Mungu kwa roho na kweli ni silaha kwa sababu kunakaribisha nguvu ya  roho mtakatifu.kupitia roho mtakatifu matando16:25-26 Paulo na sila waliomba na kumsifu Mungu mpaka milango ya gereza ikafunguka.ni kwa sababu ya sifa iliyo ya kweli na kupitia sifa watu hupata nguvu ya kufanya maombi bila kuchoka.kama mpendwa yakupasa uombee ibada ya sifa kila unapoingia ibadani ili umuone Mungu akifungua watu na kuponya watu na kunena na kanisa.

·         Radi ya Mungu,ina maanisha tupo katika ufalme usioteteleka zaburi18:13bwana alipiga radi mbinguni,yeye aliye juu akaitoa sauti yake) ,1samweli2:10(washindanao na BWANA watapondwa kabisa toka mbinguni yeye atawapigia radi) kumbe Mungu tunayemwamini ni mtetezi wetu wakati wa vita adui atakapojipanga kutupiga atasambalatishwa kwa Radi kutoka kwa MUNGU.

Matumizi ya silaha hizi yapo katika maombi na kuhudhuria ibada kwa bidii.

hivyo ninashauri utumie bidii ya hali ya juu sana katika maombi ya kawaida na kufunga mara nyingi angalau mara mbili kwa wiki au mara tatu au zaidi maana adui shetani halali vivyo nasi tusifanye kwa ulegevu.

Pia yatupasa tuhudhurie ibada isiwepo sababu yoyote yakutufanya tusiende ibadani.

Hizi ni moja silaha zinazokupa ushindi na kukufanya usimame imara  ukimtegemea MUNGU katika maisha ya kiroho.

                            MUNGU akubariki kwa kusoma ujumbe huu…




+

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni